Wewe ni Mungu

Kwaya ya Mt. Kizito Makuburi

Sikia aa sikia Bwana,
Sikia aa sikia Bwana sauti yangu
Sikia aa sikia leo
Sikia aa sikia Bwana sauti yangu.

Hii sauti inabeba hisia zangu
Zilizomo moyoni mwangu sikia Bwana sauti yangu

Naeleza furaha niliyo nayo
Na hamu ya kukushukuru sikia Bwana sauti yangu.

Nakufunulia moyo wangu uko wazi,
Nakumiminia, sifa na tenzi Mwenyezi,
Napiga kelele usikie Bwana sauti yangu

Sikia aa sikia Bwana (Mungu we)
Sikia aa sikia Bwana sauti ya moyo,
Moyo,moyo, wangu moyo, moyo, moyo ha ha-

Nimejua ya kwamba - wewe ni Mungu kila wakati
Naona wazi kwamba - wewe ni Mungu kila wakati
Kwenye furaha - wewe ni Mungu kila wakati
Na kwenye magumu bado- wewe ni Mungu kila wakati
Haupungui neno - wewe ni Mungu kila wakatii

Hukutaka raha zinipe kiburi -
Aeee eee ukanipimia.
Na taabu ziliponishambulia - -
Ukafungua (Bwana) mlango nikatoka salama.

Nimejua ya kwamba - wewe ni Mungu kila wakati
Naona wazi kwamba - wewe ni Mungu kila wakati
Kwenye furaha - wewe ni Mungu kila wakati
Na kwenye magumu bado- wewe ni Mungu kila wakati
Haupungui neno - wewe ni Mungu kila wakatii

Na vipaji ona hukunipa vyote -
Aaee eee ukanipimia.
Ingawaje nilipoweka juhudi -
Ukafungua(Bwana) mlango nikatoka salama.

Nimejua ya kwamba - wewe ni Mungu kila wakati
Naona wazi kwamba - wewe ni Mungu kila wakati
Kwenye furaha - wewe ni Mungu kila wakati
Na kwenye magumu bado- wewe ni Mungu kila wakati
Haupungui neno - wewe ni Mungu kila wakatii

Sikuumbwa msafi kama ulivyo,
Aaee eee ukanipimia.
Hata hivyo dhambi iliponisonga,
Ukafungua (Bwana) mlango nikatoka salama.

Nimejua ya kwamba - wewe ni Mungu kila wakati
Naona wazi kwamba - wewe ni Mungu kila wakati
Kwenye furaha - wewe ni Mungu kila wakati
Na kwenye magumu bado- wewe ni Mungu kila wakati
Haupungui neno - wewe ni Mungu kila wakatii

Yeyeyeye yeyeyeyeye yeyeyeyeyeeeeee

Nakuja nimebeba sifa kukuzungushia
Nakuja ninaimba wimbo watu wakutukuze
Nakuja nimebeba sifa kukuzungushia
Maana utukufu ni wako milele na milele.

Nakuja nimebeba shangwe, na chereko
Nakuja nimebeba kinanda watu wakuimbie-
Nakuja nimebeba sifa kukuzungushia
Maana utukufu ni wako milele na milele.

Nakuja nimebeba sifa kukupamba
Nakuja nimebeba maua jama watu wakutukuze-
Nakuja nimebeba sifa kukuzungushia
Maana utukufu ni wako milele na milele.

Milele na milele, milele na milele,
Milele na milele,milele ni Mungu wa pekee...

* (Bass) Wewe ni Mungu, wewe ni Bwana,
We ni mwema, utabaki Mungu
* (Tenor) wewe ni wa kwanza ni Mungu weee, wewe ni wa mwisho eee
Unaitwa Alfa ni Mungu wee, wewe ni Omega eee